Thursday, 12 July 2018

Friday, 22 June 2018

Yanga yamalizana na Mbenini
Na George Mganga Imeelezwa kuwa Mshambuliaji mpya wa Yanga kutoka Benin, Marcelin Koukpo tayari amefanyiwa vipimo vya afya na sasa yu tayari kuanza mazoezi na kikosi kuanzia wiki ijayo. Taarifa zinaeleza kuwa Koukpo tayari alishawasili nchini muda mrefu na panapo majaaliwa wiki ijayo ataungana na wachezaji wenzake kuanza kujifua kuelekea mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika. Daktari wa Yanga, Edward Bavu amekamilisha kumfanyia vipimo hivyo Koukpo ambaye alikuwa anaichezea Les Buffles ya nchini kwao kabla kujiunga na Yanga na kuonekana yupo fiti kiafya. Koukpo tayari ameshamalizana na mabosi wa Yanga kupitia Mwenyekiti wa usajili, Hussein Nyika kwa kusaini mkataba wa miaka miwili. Baada ya kukamilisha vipimo kwa mchezaji huyo, inaelezwa kuwa Yanga ipo kwenye mazungumzo na wachezaji wengine ikiwemo Mohamed Ibrahim wa Simba ambaye alikosekana katika michezo mingi ya msimu uliomalizika

Monday, 11 June 2018

Tarimba Abas anena kuhusu kamati yake
“ tumesikia wachezaji baadhi tu ndio wana mikataba na klabu kwa sasa wengi mikataba yao imekwisha. Jukumu la kamati yetu kwanza kabisa ni kurudisha heshima ya Yanga nchini pia kuifanya timu ya ushindani kimataifa. Tutakutana haraka kuona nini kifanyike ili kuipa nguvu timu. Nguvu ya timu ni ubora wa wachezaji na bechi la ufundi kwa matokeo chanya. Si kazi ndogo lakini tutahakikisha tunafanya kile tunachoweza kwa dhamana tuliyopewa na wanachama na Mungu atasaidia. Kikubwani ushirikiano pande zote kwa masilahi mapana ya klabu.‘ - Tarimba Abbas

Sunday, 10 June 2018

WANACHAMA YANGA WAMREJESHA MANJI MADARAKANI, TARIMBA APEWA JUKUMU LA KUSAJILI WACHEZAJI WAPYA
WANACHAMA wa klabu ya Yanga kwa kauli moja wamekubaliana kumrejesha madarakani, Mwenyekiti wao Yussuf Mehboob Manji katika mkutano Mkuu wa mwaka uliofanyika Bwalo la Maafisa wa Jeshi la Polisi, Oysterbay, Dar es Salaam leo. Pamoja na kumrejesha Maji aliyejiuzulu Mei mwaka jana, wanachama hao wameunda Kamati ya watu tisa chini ya Rais wa zamani wa klabu, Tarimba Abbas kusimamia usajili na mambo mengine muhimu ya klabu kwa sasa. Akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya mkutano huo, Kaimu Katibu Mkuu, Charles Boniface Mkwasa amesema kwamba agizo la Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harison Mwakyembe kufanyika kwa uchaguzi wa kuziba nafasi za viongozi waliojiuzulu ndani ya miezi miwili pia linafanyiwa kazi. Wanachama wa Yanga kwa kauli moja wamekubaliana kumrejesha madarakani, Mwenyekiti wao Yussuf Manji Mkwasa pia amesema kwamba wameridhia mwongozo wa mabadiliko ya uendeshwaji wa klabu kwa kuingia kwenye soko la hisa na kwamba mchakato wa zoezi hilo unashughulikiwa na Wakili maarufu, Alex Mgongolwa. Mapema akifungua mkutano huo, Waziri Mwakyembe pamoja na kuipongeza Yanga kwa klabu yenye mafanikio makubwa nchini, pia aliwapa miezi wawe wamefanya uchaguzi ili kuziba mapengo ya viongozi walioondoka. Waziri Mwakyembe amesema Yanga inahitaji kuwa na uongozi imara utakaosajili wachezaji wazuri wa kuirejeshea heshima klabu kwa kufanya vizuri kwenye mashindano. “Mkifanikiwa Yanga, nimefanikiwa mimi kama Serikali...mnatakiwa kupata kundi la wanachama ambao mtasaidiana kuvuka katika kipindi hiki cha mpito,”amesema. Aidha, Mwakyembe amewataka wale wanaopinga mabadiliko ya mfumo wa uendeshwa wa klabu hiyo kufika kwenye mkutano kutoa ya moyoni na wakishindwa wamfuate ofisini kwake. Pamoja na Waziri Mwakyembe, Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Huruma Mkuchika ambao walianza kwa kikao cha faragha na uongozi wa Yanga chini ya Kaimu Mwenyekiti, Clement Sanga. Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Mkurugenzi wa Michezo, Yusuph Singo, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya, Jaji John Mkwawa na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu pamoja na Katibu Mkuu, Charles Boniface Mkwasa. Manji aliingia Yanga mwaka 2006 kama mdhamini kupitia kampuni yake ya Lotto Kitita, lakini baadaye akawa mfadhili Mkuu wa klabu kabla ya kuwa Mwenyekiti. Katika kipindi chake cha kuwa mfadhili na Mwenyekiti wa Yanga, Manji aliifanyia mengi klabu– kubwa ni kuirejeshea hadhi na heshima klabu hiyo. Alipoingia mwaka 2006 aliikuta klabu ipo dhoofu kiuchumi na haiwezi kushindana na mahasimu wao, Simba katika kuwania wachezaji bora ambao ndiyo mtaji wa kushinda mataji. Wakati huo Yanga ilikuwa inasajili wachezaji ambao ama walikuwa wameachwa na timu zao, waliojipeleka wenyewe kwa mapenzi yao au waliopatikana kwa njia ya mchujo wa majaribio. Lakini mara baada ya Manji kuingia Yanga, klabu hiyo ikaanza kusifika kwa kusajili wachezaji wa kigeni na wale nyota wa hapa nyumbani, ikiwa ni pamoja na kubomoa ngome ya mahasimu, Simba SC. Mwaka 2009 fedha za Manji zilimtoa kipa kipenzi cha wana Simba Msimbazi, Juma Kaseja na desturi hiyo ikaendelea baadaye wakichukuliwa beki Kelvin Yondan na mshambuliaji Mganda Emmanuel Okwi. Yanga iliipiku Simba ‘kimafia’ katika kumsajili beki anayeweza kucheza kama kiungo pia, Mbuyu Twite kutoka APR ya Rwanda, tu kwa jeuri ya fedha. Aliyekuwa Mwenyekiti wa Simba, Alhaj Ismail Aden Rage alianza kuonekana akimsainisha Mbuyu mjini Kigali, lakini baadaye Mwenyekiti wa Usajili wa timu ya Jangwani, Abdallah Bin Kleb akaingia kwa ‘gia kubwa’ na kubadilisha mambo, Mbuyu akatua Jangwani. Na ni katika kipindi hicho imeshuhudiwa Manji amewazima kabisa Simba na Yanga ikitawala soka ya Tanzania na kuzidi kujiongezea mashabiki na wapenzi. Lakini migogoro haikukosekana pia wakati wa utawala wa Manji, ambayo wakati fulani iliiathiri timu mfano ule wa kutaka kumng’oa aliyekuwa Mwenyekiti, Wakili Lloyd Nchunga ulioiponza klabu ifungwe 5-0 na mahasimu, Simba Mei 6, mwaka 2012. Mapema mwaka jana, Manji alikuja na mpango wa kutaka kujikodisha klabu kupitia kampuni aliyoisajili kwa jina la Yanga Yetu, lakini ukapata upinzani mkali na kuamua kuachana nao. Kabla ya kufikia maamuzi haya, Manji alipitia kwenye misukosuko na Serikali kuanzia Januari hadi Aprili, kwanza akikamatwa na kuwekwa ndani kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya na baadaye akidaiwa kumiliki pasipoti mbili. Kwa sasa klabu inakabiliwa na hali ngumu kiuchumi kiasi cha kuambulia ushindi wa mechi moja kati ya 14 zilizopita, nyingine saba wakifungwa zote na kushinda 1
Alichokisema Papy Tshishimbi kuhusu kujiunga Simba
Kiungo Papy Tshishimbi ameondoka nchini na kurejea kwao DR Congo kwa ajili ya mapumziko. Tshishimbi amekuwa akihusishwa na kujiunga na Simba, jambo ambalo limewapa hofu na hasira baadhi ya mashabiki wa Yanga. Tshishimbi hakuwa amewahi kulizungumzia suala hilo lakini jana amekutana na Salejembe jijini Nairobi, Kenya na kuweka wazi kila kitu. Tshishimbi amesema anareja kwao kwa mapumziko akiwa bado ni mchezaji wa Yanga na atarejea baada ya mapumziko. Kuhusiana na suala la Simba, hii ndiyo kauli yake. “Kuhusu Simba ninasikia tu kwa kweli. Lakini hakuna ambaye amewahi kunifuata tukalizungumzia suala hilo.” Alipoulizwa kama Simba wakimfuata, yuko tayari kujiunga nao? “Soka ni biashara rafiki yangu, unajituma na kufanya vizuri ili upae kibiashara na kujiendeleza zaidi. Timu ikifanikiwa, soko linakuwa juu. “Kama Simba wananihitaji, niko tayari wanaweza kusema wanahitaji nini nami niangalie.”

Saturday, 9 June 2018

Kuelekea mkutano mkuu wa Yanga Leo Akilimali atoa kauli hii...
Kuelekea Mkutano Mkuu wa Yanga unaofanyika Jumapili ya leo katika ukumbi wa Police Officers Mess jijini Dar es Salaam, Katibu wa Baraza la Wazee wa klabu hiyo, Ibrahim Akilimali ametoa neno lake. Mzee huyo ambaye awali alionekana kupinga mabadiliko hayo amesema kuwa kwa sasa anayaunga mkono kwa asilimia zote. Akilimali ameeleza kuwa mabadiliko Yanga kwa sasa hayakwepeki kutokana na timu yao ilipofikia hivi sasa mpaka kwa mwenendo ilionao kuwa si mzuri. Kiongozi huyo amesema yeye hajawahi kupinga mabadiliko bali alikataa mfumo ambao alikuja nao Yusuph Manji hapo awali akitaka kukodisha timu na nembo jambo ambalo amefunguka kwa kueleza halikuwa sahihi kwake hata kidogo. Ikumbukwe wakati Manji akiwa Mwenyekiti Yanga, alikuja na ombi la kutaka Yanga aikodishe akihitaji timu na nembo na baadhi ya wanachama ikiwemo Akilimali na wengine kuibuka na kupinga kwa nguvu suala hilo. Mkutanoo Mkuu wa Yanga unatarajia kuanza leo majira ya saa 4 kamili za asubuhi ambapo Waziri mwenye dhamana ya michezo, Harrison Mkwayembe anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.
Matola kocha mpya Simba
Baada ya Simba kumtimua Kocha Mkuu, Mfaransa, Pierre Lechantre, mabosi wa timu hiyo wamefikia uamuzi wa kuikabidhi timu hiyo kwa Mrundi, Masoud Djuma Irambona ambaye atasaidiwa na mkongwe, Selemani Matola. Djuma ambaye ndiye kocha msaidizi wa Simba kwa sasa, yupo na kikosi hicho mjini hapa Nakuru ambapo Simba inajiandaa kucheza mchezo wa fainali ya michuano ya SportPesa Super Cup dhidi ya Gor Mahia, kesho Jumapili. Alhamisi ya wiki hii, mabosi wa Simba walimpiga chini Mfaransa huyo baada ya kushinikiza kupewa mkataba mpya licha ya kuambiwa asubiri mpaka timu itakaporudi Dar. Lechantre alitofautiana na vigogo wa Simba baada ya kushinikiza mabadiliko makubwa kwenye mkataba wake ikiwemo mshahara wa Sh 90milioni kwa mwezi pamoja na kupandishiwa posho zote na hata ndege asafiri kwenye daraja la kwanza. Kwa mujiv=bu wa gazeti la Championi limedokezwa na kiongozi mkubwa wa Simba kwamba baada ya timu hiyo kuwasili jijini Dar ikitokea Kenya, Djuma atatangazwa kama kocha mkuu huku msaidizi wake akiwa Matola ambaye msimu uliopita alikuwa kocha msaidizi wa Lipuli ya Iringa. Matola ndiye nahodha wa mwisho kuipeleka Simba kwenye robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu wa 2003. “Tumeamua kumuongeza Matola kwenye kikosi chetu kwa kuw atuna imani naye hivyo atakuwa msaidizi chini ya Djuma, tumepanga kumtambulisha mara tu tutakaporejea Tanzania. “Kwa sasa tumeamua kufanya hivyo kwani tumeona ni bora kuwatumia makocha wa Kiafrika zaidi hasa wa ukanda wetu huu ambao wanajua vizuri staili ya soka letu kuliko Wazungu,” kilisema chanzo. Alipotafutwa Matola alisema: “Bado sijapata taarifa kuhusiana na hilo lakini tungoje kwanza nitaweka wazi baadaye.” Hakuna kiongozi wa Simba aliyekuwa tayari kuzungumzia ishu hiyo jana kwa kutajwa jina, huku wengi wakidai watatoa ufafanuzi baadaye.