FERNANDO TORRES AMSHAURI GRIEZMANN KUZITOSA BARCELONA NA MAN UNITED
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alitaka kuondoka Hispania kutua Old Trafford majira ya joto, na alipewa nafasi kubwa kuondoka.
Fernando Torres amekiri kuwa anaamini Atletico Madrid wanaweza kumshawishi Antoine Griezmann kubaki klabuni hapo, licha ya Barcelona na Manchester United.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alitaka kuondoka Hispania kutua Old Trafford majira ya joto, na alipewa nafasi kubwa kuondoka.
Atleti walipewa adhabu ya kufungiwa usajili na mshambuliaji huyo muhimu alijifunga kwa mkataba mpya, lakini Barca wameibuka kuwa klabu yenye nafasi kubwa kuipata saini yake.
Hata hivyo, Torres sasa amemtaka mchezaji mwenzake huyo kufikiria kuzikataa klabu hizo badala yake aendelee kubaki Wanda Metropolitano.
"Griezmann bado yupo na sisi na ni budi tumfurahie," alikiambia Marca. "Atletico wanaweza kusajili na kushikilia wachezaji bora.
"Ningependa kama Griezmann angetaka kubaki Atletico. Ni vema kumuuliza [kama anataka kubaki], lakini atakapoamua kubaki, itakuwa kwa sababu amependa."
Inasadikika kuwa Atletico wameiripoti Barcalona kwa FIFA kwa kukiuka utaratibu kumfuatilia nyota wao Griezmann.
0 coment�rios: